Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti 21, 2016

Tangazo

Wapendwa,masomo nitaendelea kuyatuma kuanzia ijumaa tarehe 26/08/2016

Kesha la Asubuhi Agosti 24 2016

Agosti 24 Rehema na HakiVilikutana Msalabani Fadhili na kweli zimekutana, Haki na amani zimehusiana. Zaburi 85:10.             Haki na rehema vilisimama mbalimbali, vikipingana kila kimoja na kingine, vikitenganishwa na ufa mkubwa. Bwana Mkombozi wetu aliuvisha uungu wake kwa ubinadamu na kutenda kwa niaba ya watu, tabia ambayo haikuwa na doa wala waa. Alikita msalaba wake katikati ya mbingu na dunia na kuufanya kuwa kivutio ambacho kilifika sehemu zote mbili, kikivuta Haki na Rehema toka pande zote zinazogawanywa na ufa ule.... Hapo huo msalaba ulionayeye aliye sawa na Mungu akiibeba adhabu kwa ajili ya dhuluma na dhambi zote. Kwa kuridhika kikamilifu, Haki ihinama kwa kicho mbele ya msalaba, ikisema, imetosha.              Kwa sadaka iliyofanywa kwa niaba yetu tunakuwa tumewekwa mahali pazuri sana. Mwenye dhambi, anapovutwa kwa uwezo wa Kristo kutoka katika uta...

Biblia kwa mpango Agost 24 2016

Ezra 7 1  Ikawa baada ya mambo hayo, wakati wa kutawala kwake Artashasta, mfalme wa Uajemi, Ezra, mwana wa Seraya, mwana wa Azaria, mwana wa Hilkia,  2  mwana wa Shalumu, mwana wa Sadoki, mwana wa Ahitubu,  3  mwana wa Amaria, mwana wa Azaria, mwana wa Merayothi,  4  mwana wa Zerahia, mwana wa Uzi, mwana wa Buki,  5  mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni, kuhani mkuu;  6  huyo Ezra akakwea kutoka Babeli; naye alikuwa mwandishi mwepesi katika sheria ya Musa, aliyokuwa ameitoa Bwana, Mungu wa Israeli; naye mfalme akamjalia matakwa yake yote, kama mkono wa Bwana, Mungu wake, ulivyokuwa pamoja naye.  7  Nao wakakwea baadhi ya wana wa Israeli, na wa makuhani, na wa Walawi, na waimbaji, na mabawabu, na Wanethini, ili kwenda Yerusalemu, katika mwaka wa saba wa mfalme Artashasta.  8  Naye Ezra akafika Yerusalemu mwezi wa tano katika mwaka wa saba wa huyo mfalme.  9  Maana alia...

Lesson Jumatano Agosti 24 2016

Dorkasi Kule Yafa Soma Matendo 9:36-42. Dorkasi alifanya nini alipoona kuwa alikuwa amezungukwa na wahitaji? Msemo huu unamaanisha nini “waaminio, hasa wajane?” Matendo 9:36-42 36   Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa.   37   Ikawa siku zile akaugua, akafa; hata walipokwisha kumwosha, wakamweka orofani.   38   Na kwa kuwa mji wa Lida ulikuwa karibu na Yafa, nao wanafunzi wamesikia ya kwamba Petro yuko huko, wakatuma watu wawili kwake, kumsihi na kusema, Usikawie kuja kwetu.   39   Petro akaondoka akafuatana nao. Alipofika, wakampeleka juu orofani wajane wote wakasimama karibu naye, wakilia na kumwonyesha zile kanzu na nguo alizozishona Dorkasi wakati ule alipokuwa pamoja nao.   40   Petro akawatoa nje wote, akapiga magoti, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, ondoka. Naye akafumbua ma...

Kesha la Asubuhi,Agosti 22,2016

Kristo Alistahimii Msalaba kwa Ajili Yetu Tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, aljinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Wafilipi 2:8.             Kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye milele ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu. Alikufa msalabani kama kafara kwa ajili ya ulimwengu na kupitia kwa kafara yake ndipo baraka kuu inapokuja arnbayo Mungu anatupatia, -- karama ya Roho Mtakatifu. Baraka hii ni kwa ajili ya wote watakaompokea Kristo.            Ulimwengu ulioanguka ni eneo la mapambano kwa ajili ya pambano kuu kabisa ambalo viumbe vyote vya mbinguni na vya duniani vimewahi kushuhudia. Sehemu hii iliteuliwa kama ukumbi wa maonesho ambapo pambano kuu kabisa lingepiganwa kati ya wema na uovu, kati ya mbingu na kuzimu. Kila mwanadamu ana sehemu ya kufanya katika pambano hili. Hakun...

Biblia Kwa Mpango Ezra 5,Agosti 22,2016

Ezra  5 1  Basi manabii, Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido, wakawafanyia unabii Wayahudi waliokuwako Yerusalemu na Yuda; waliwafanyia unabii kwa jina la Mungu wa Israeli.  2  Ndipo akaondoka Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na Yoshua, mwana wa Yosadaki, wakaanza kuijenga nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu; na pamoja nao walikuwa manabii wa Mungu, wakiwasaidia.  3  Wakati ule ule Tatenai, liwali wa ng'ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzi wao, wakawajia, wakawaambia, Ni nani aliyewapa amri kuijenga nyumba hii, na kuumaliza ukuta huu?  4  Ndipo wakawauliza hivi, Majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani na nani?  5  Lakini jicho la Mungu lilikuwa likiwaelekea wazee wa Wayahudi, hao wasiwazuie, hata habari ile imfikilie Dario, ndipo jawabu litakapopatikana kwa waraka.  6  Hii ndiyo nakala ya waraka waliyompelekea mfalme Dario; na Tatenai, liwali wa ng'ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzake wa Kiajemi, waliokuwako h...

JumatatuAgost 22,2016 Lesson

Nikusaidieje? Soma: Marko 10:46-52 na Yohana 5:1-9. Katika matukio yote mawili, Yesu   aliuliza maswali. Kwa nini alifanya hivyo? Marko 10:46-52 46   Wakafika Yeriko; hata alipokuwa akishika njia kutoka Yeriko, pamoja na wanafunzi wake, na mkutano mkubwa, mwana wa Timayo, Bartimayo, yule mwombaji kipofu, alikuwa ameketi kando ya njia.   47   Naye aliposikia ya kwamba ni Yesu Mnazareti, alianza kupaza sauti yake, na kusema, Mwana wa Daudi, Yesu, unirehemu.   48   Na wengi wakamkemea ili anyamaze, lakini alizidi kupaza sauti, Mwana wa Daudi, unirehemu.   49   Yesu akasimama akasema, Mwiteni. Wakamwita yule kipofu, wakamwambia, Jipe moyo; inuka, anakuita.   50   Akatupa vazi lake, akaruka, akamwendea Yesu.   51   Yesu akamjibu, akamwambia, Wataka nikufanyie nini? Yule kipofu akamwambia, Mwalimu wangu, nataka nipate kuona.   52   Yesu akamwambia, Enenda zako, imani yako imekuponya. Mara akapata ku...

Kesha Agosti 22,2016

Picha