Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti 28, 2016

Lesson Agosti 27-Sept 2,2016

Picha
Somo la 10                                                Agosti 27 — Septemba 2   Yesu Aliwafanya Wamwamini   Usomaji wa Biblia: Ezra 10   Sabato Mchana   Soma kwa Ajili ya Somo la Juma Hili: Mwa. 15:6; Hes. 11:4; 1 Kor. 3:1-9;   Dan. 6:1-3; Neh. 2:1-9; Kum. 4:1-9; Mdo. 2:42-47.   Fungu la Kukariri: “Lakini habari zake zikazidi kuenea, wakakutanika makutano mengi wamsikilize na kuponywa magonjwa yao.” (Luka5:15). K wa miaka kadhaa, Kanisa moja la Waadventista wa Sabato limekuwa likitoa kifungua kinywa siku tano kwa juma kwa shule ya awali ya mahali pale. Ijapokuwa serikali ya taifa lile ilikuwa ya kiraia kabisa (haikuwa ya kidini), ililazimika kupitisha sheria ili kutoa pesa ya kutosha k...

Kesha la Asubuhi agosti 27-sept 2,2016

Agosti 27 Tunabeba Msalaba na Kujikana Nafsi Nimesulubiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo ya hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu. Wagalatia 2:20.         Kristo alisulubiwa kwa ajili ya mwanadamu aliyeanguka dhambini. Lakini kwa wengi wanaojiita kuwa ni Wakristo, tukio hili halina maana yoyote. Kwa matendo, wanaukana msalaba wa Kristo ... Wanakubali kuwa Kristo alikufa msalabani, lakini kwa sababu kuna uzoefu wa kusulubiwa ambao inawapasa waupitie, hawapokei mafundisho yatakayowafanya wajikane nafsi na kujitoa. Hawa ni Wakristo kwa jina tu. Kiini cha imani yao sio Mwokozi aliyesulubiwa, anayewaletea wote wanaompokea fadhila ya kuwa wana na binti za Mungu.         Acha anasa za dhambi na badala yake uichukue mbingu na uzima wa milele. Siku chache...

Usomaji wa Biblia Kwa mpango Agosti 28-sept 2

Ezra 10 1  Basi hapo Ezra alipokuwa akiomba na kuungama, akilia, na kujiangusha kifudifudi mbele ya nyumba ya Mungu, wakamkusanyikia katika Israeli wote kusanyiko kubwa sana la wanaume, na wanawake, na watoto; maana watu hao walikuwa wakilia sana.  2  Hata Shekania, mwana wa Yehieli, mmoja wa wana wa Elamu, akajibu, akamwambia Ezra, Sisi tumemkosa Mungu wetu, nasi tumeoa wanawake wageni wa watu wa nchi hizi; lakini kungaliko tumaini kwa Israeli katika jambo hili.  3  Haya basi! Na tufanye agano na Mungu wetu, kuachana na wake zetu, na wale waliozaliwa nao, tukilifuata shauri la bwana wangu, na shauri la hao wanaoitetemekea amri ya Mungu wetu; mambo haya na yatendeke kwa kuifuata torati.  4  Inuka; maana shughuli hii yakuhusu wewe; na sisi tu pamoja nawe; uwe na moyo mkuu, ukaitende.  5  Ndipo Ezra akaondoka, akawaapisha wakuu wa makuhani, na Walawi, na Israeli wote, ya kwamba watafanya kama hayo. Basi wakaapa.  6  Kisha Ezra a...