Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 22, 2017

januari28-Talanta Zilizotumiwa Vibaya

Talanta Zilizotumiwa Vibaya Na jina la nduguye aliitwa Yubali; huyo ndiye baba yao wapigao kinubi na filimbi. Sila naye akamzaa Tubal-kaini, mfua kila chombo cha kukatia, cha shaba na cha chuma. Mwanzo 4:21, 22. Kwenye Gharika uvumbuzi Wa sanaa na ustadi wa binadamu ulioangamia ulikuwa wa juu kuliko dunia inavyojua leo. Sanaa iliyoangamizwa ilikuwa zaidi ya sanaa inayofikiria ambayo ulimwengu unajivunia leo. ... Alipokuwa akiuangalia ulimwengu, Mungu aliona kwamba akili aliyokuwa amewapa watu ilikuwa imepotoshwa, kwamba fikra za moyo wake zilikuwa ovu wakati wote. Mungu alikuwa amewapatia watu hawa ujuzi. Alikuwa amewapatia mawazo ya thamani, ili wapate kukamilisha mpango wake. Lakini Bwana aliona kuwa wale aliowaumba ili wawe na hekima, busara na uamuzi, walikuwa wakitumia kila uwezo wa akilj zao kutukuza nafsi. Kwa kutumia maji ya Gharika, alifutilia mbali jamii hii iliyokuwa ikiishi muda mrefu kutoka katika dunia na pamoja nao ukaangamia ujuzi amba...

januari27-Majitu Katika Nchi

Majitu Katika Nchi Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile. Mwanzo 6:4. Watu wa kwanza duniani walipokea maelekezo yao kutoka kwa huyo Mungu asiye na mwisho ambaye aliiumba dunia. Wale waliopokea ujuzi wao moja kwa moja kutoka kwa hekima isiyo na mwisho hawakupungukiwa hekima... Yapo mavumbuzi mengi na maendeleo na mashine zinazofanya kazi leo ambazo watu wa kale hawakuwa nazo. Hawakuzihitaji... Watu kabla  ya gharika waliishi miaka mamia mengi na walipokuwa na umri wa miaka mia, walifikiriwa kuwa vijana tu. Wale watu walioishi maisha marefu walikuwa na akili nzuri na wenye miili mizuri... Walianza kuonekana kwenye jukwaa la shughuli katika umri wa miaka sitini hadi miaka mia moja, umri ambao kama ilivyo leo, wale ambao wameishi maisha marefu wanakuwa wamekwisha kufanya sehemu yao katika kipindi kifupi sana cha maisha na wanakuwa wameshaondoka jukwaani. Walikuwepo majitu wengi, watu warefu na wenye nguvu, waliofahamika kwa hekima, wenye ustadi...

Januari 26 - Mungu au Sanamu?

Mungu au Sanamu? Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu... Wazfanyao watafanana nazo, Kila mmoja anayezitumainia. Zaburi 115:4-8. Siku za Nuhu laana maradufu ilikuwa duniani ikiwa ni matokeo ya uasi wa Adamu na ya mauaji yaliyofanywa na Kaini. Hata hivyo, haya yalikuwa hayajabadilisha sana uso wa asili wa dunia. . . jamiii ya binadamu bado ilikuwa katika nguvu zake za awali. Vizazi vichache tu vilikuwa vimepita tangu Adamu alipoweza kuufikia mti ambao ulikuwa na uwezo wa kurefusha uhai; na urefu wa maisha ya mwanadamu ulikuwa bado ukipimwa kwa karne. Kama watu hawa walioishi maisha marefu wakiwa na nguvu zisizo za kawaida katika kupanga na kutenda, wangejitoa wenyewe kwa ajili ya utumishi wa Mungu, wangefanya jina la Muumba wao liwe sifa katika dunia... Lakini walishindwa kufanya hili. ... Wakiwa hawakutamani kumfanya Mungu abaki katika ujuzi wao, wakafikia hatua ya kukana kuwepo kwake. Wakatukuza viumbe ...

Januari 25 -Mlango Ulio Wazi

Kwa imani Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu alimhamisha; maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu. Waebrania 11:5. Tutakapojifunza kuenenda kwa imani na wala sio kwa hisia, tutapata msaada kutoka kwa Mungu wakati ule ule tunapouhitaji na amani itatujia mioyoni mwetu. Ilikuwa ni maisha haya sahili ya utiifu na kutuinaini ambayo Henoko aliishi. Tukijifunza somo hili la kutumainia kusiko na makuu, tutapata ushuhuda alioupata, kwamba alimpendeza Mungu. Katika kila hatua ya kujenga tabia yako inakupasa umpendeze Mungu. Unaweza kufanya hili; kwani Henoko alimpendeza japo akiishi katika kizazi kilichojaa upotovu. Na wapo akina Henoko katika siku zetu hizi. Kwa miaka mia tatu Henoko alikuwa akitafuta usafi wa moyo, iii apate kuwa katika upatanifu na mbinguni. Kwa kame tatu alikuwa akiternbea na Mungu. Siku kwa siku alikuwa akitamani kuwa katilca uhusiano wa ...

Januari 24- Kumtazama Kristo

Kumtazama Kristo Lakini sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama vile katika kioo, tunabadiishwa tufanane na mfano ito hito, toka utukufu hala utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho. 2 Wakorintho 3:18. Katikati ya maisha ya kazi nyingi, Henoko kwa uthabiti alidumisha mawasiliano yake na Mungu. Kadiri kazi zake zilivyozidi kuwa kubwa na zenye kushinikiza, ndivyo sala zake zilivyozidi kuwa za dhati na za kudumu. Aliendelea kujitengarnwenyewe kutoka katika jamii nyakati fulani. Baada ya kukaa kwa muda fulani kati ya watu, akifanya kazi ya kuwanufaisha kwa mfano na maelekezo, huwa alikuwa akiondoka, ili atumie muda akiwa peke yake, mwenye njaa na kiu ya ule ujuzi ambao Mungu mwenyewe ndiye awezaye kuutoa. Akiwasiliana hivyo na Mungu, Henoko alifikia hatua ya kuakisi sura ya Mungu zaidi na zaidi. Uso wake uling’aa kwa nuru takatifu, naam, nuru ing’aayo usoni pa Yesu. Alipotoka kwe...

Januari 23- Mungu Alimtwaa

Mungu Alimtwaa Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa. Mwanzo 5:24. Tunasoma kuwa Henoko, alitembea na Mungu kwa miaka mia tatu. Huo ulikuwa ni muda mrefu wa kuwa na ushirika nae... Aliwasiliana na Mungu kwa sababu ilikubalika kwake, .. .naye alipenda jamii ya Mungu. Henoko alikuwa mtu ambaye hakujificha. Wapo wengi wanaoya tazama maisha yake kama ya namna ambayo kwa ujumla binadamu wa kawaida hawawezi kufikia. Lakini maisha na tabia ya Henoko... inawakilisha kile ambacho maisha na tabia za wote yapasa ziwe, ikiwa tunataka kuwa tayari kubadilishwa kama Henoko alivyokuwa, wakati Kristo atakapokuja. Maisha yake yalikuwa kile ambacho kila mmoja anaweza kuwa kama akiungana kabisa na Mungu. Inatupasa tukumbuke ya kwamba Henoko alikuwa amezingirwa na mivuto potovu sana kiasi kwamba Mungu alileta gharika ya maji duniani kuangamiza wakazi wake kwa sababu ya ufisadi wao. Tunaishi katika kizazi kiovu. Hatari za siku za mwisho zinàzi...