Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 15, 2017

Januari 22- Alitembea Pamoja na Mungu

Alitembea Pamoja na Mungu Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela. Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu. Mwanzo 5:21, 22. Kuhusu Henoko imeandikwa kwamba aliishi miaka sitini na mitano, akazaa mwana... Katika miaka hii ya awali Henoko alikuwa amempenda na kumcha Mungu na alikuwa amezishika amri zake... Lakini baada ya kuzaliwa kwa mwana wake wa kwanza, Henoko alifikia kiwango cha juu zaidi cha uzoefu; alivutwa kuwa katika uhusiano wa karibu zaidi na Mungu. Kwa ukamilifu zaidi alitambua majukumu yake binafsi na wajibu kama mwana wa Mungu. Alipoona upendo wa mwana kwa baba yake, usahili wake wa kutegemea ulinzi wake; alipojisikia upendo wenye shauku, wenye kina uliotoka moyoni mwake kwa ajili ya mwana wake wa kwanza, aljifúnza somo la pekee la upendo wa ajabu wa Mungu kwa watu katika karama ya Mwana wake na ujasiri ambao watoto wa Mungu wanaweza kuwa nao katika Baba yao wa r...

Januari 21 - Kaini “Akatoka”

Kaini “Akatoka” Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana. Mwanzo 4:16. Mungu alikuwa amempa Kaini fursa ya kuungama dhambi yake... Alijua ukubwa wa kitendo alichokuwa ametenda na pia uongo aliokuwa amesema katika kuficha; lakini bado alikuwa mwasi na hukumu isingeweza kuahirishwa zaidi... Bila kujali kwamba Kaini alistahili hukumu ya kifo kulmgana na uhalifu aliotenda, bado Muumba-ji mwenye rehema aliokoa maisha yake na kumpatia fursa ya kutubu. Lakini Kaini aliishi akiendelea kuufanya moyo wake kuwa mgumu, akiendelea kutia moyo uasi dhidi ya mamlaka ya Mungu na kuwa kichwa cha safu ya wenye dhambi jasiri, walioachwa. Huyu mwasi mmoja, akiongozwa na Shetani, akawa mjaribu wa wengine; na mfano na mvuto wake ukaleta nguvu ya kuharibu tabia, hadi nchi ikawa imeharibika na kujazwa na vurugu kiasi cha kusababisha uangamivu wake... Alipopata laana ya Mungu, Kaini aliondoka nyumbani kwa baba yake... Alikuwa ametoka usofli pa Bwana, a...

Januari 20 - Uso Wako Unaonesha

Uso Wako Unaonesha Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana? Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea miangoni, nayo inakutamani wewe, walakiniyapasa uishinde. Mwanzo 4:6, 7. Bwana aliona ghadhabu ya Kaini. Aliona uso wake ulivyokosa furaha. Hivyo ni dhahiri jinsi Bwana anavyoona kila tendo kwa karibu, nia na makusudio yote, ndiyo, hata mwonekano wa uso. Japo mtu anaweza asiseme chochote, hali hii inaweza kutamka kukataa kwake kufuata njia na kutenda mapenzi ya Mungu. Hebu tazama maneno ya Bwana... Swali hili linaweza kuelekezwa kilakijanawakiume nawa kike ambaye, kama Kaini, anadhihirisha uku... anapotenda kulingana na uchochezi wa Shetani, ambao )ja kwa moja huwa unakuwa ni kinyume na masharti ya Mungu. Ukichagua kutupilia mbali mvuto mtakatifu wa ile kweli unaozuia enda yasiyofaa, Shetani atakufanya kuwa mtumwa wa mapenzi Utakuwa katika hatari ...

Januari 19- Njia Mbili za Kufuata

Njia Mbili za Kufuata Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake; bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana. Mwanzo 4:4,5. Kaini alikuja mbele za Mungu huku akinung’unika na udanganyifu moyoni mwake kulingana na kafara iliyoahidiwa na umuhimu wa sadaka za kafara. Sadaka yake haikuonesha toba yoyote kwa dhambi. Alijisikia, kama wengi wanavyojisikia leo, kwamba itakuwa ni kukubali udhaifu kufuata mpango halisi kama ulivyotolewa na Mungu, wa kutumainia wokovu wake kikamilifu kwa upatanisho wa Mwokozi aliyeahidiwa. Alichagua mpango wa kujitegemea mwenyewe. Aliamua kuja kwa stahili zake mwenyewe. Hakuleta mwanakondoo na kuchanganya damu yake na sadaka yake, lakini aliamua kuwasilisha matunda yake, mavuno ya kazi yake. Aliwasilisha sadaka yake kana kwamba anamtendea wema Mungu, ambao kupitia kwa huo alitegemea kupata kibali cha Mungu. Kaini alitii katika hatua ya kujenga madhabahu...