Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti 7, 2016

Kesha la Asubuhi Agost 13- 19 ,2016

Agosti 13 Inatupasa Tusionee Fahari Watu     Na tena, Bwana anayafahamu mawazo ya wenye hekima ya kwamba ni ya ubatili Basi, mtu ye yotee na asijisifie wanadamu. 1 Wakorintho 3 :2 0,21. Tunaishi katika kipindi cha upotovu na wanaume kwa vijana ni jasiri katika dhambi. Vijana wetu wasipolindwa kwa utakatifu, wasipolindwa kwa kanuni thabiti, uangalizi mkubwa usipodhihirishwa katika kuchagua rafiki zao pamoja na machapisho yanayolisha akili, watakuwa wameachiliwa kwa jamii ambayo maadili yao yamechafuka kama yalivyokuwa ya wakazi wa Sodoma... Vijana wetu watakutana na majaribu kila upande na ni lazima waelimishwe kwamba itawapasa wategemee nguvu itokayo juu, mafundisho kutoka juu, kuliko yale yatolewayo na binadamu. Kila mahali wapo wale wanaomdharau Bwana wetu, ambao kwa mazoea hubeza Ukristo... Wale wasio na nguvu ya kimaadili hawawezi kusimama kidete kulinda ukweli; hawana ujasiri wa kusema: “Mazungumzo ya namna hiyo yasipokoma, siwezi kusalia hapa pamoja nawe....

Somo 8:Yesu Alionesha Huruma Agosti 13-19,2016

Picha
               Yesu Alionesha Huruma                                                                                               Usomaji wa Biblia: 2 Nyakati 32Agosti 13 Sabato Mchana Soma kwa Ajili ya Sorno la Juma Hill: 2 Fal. 13:23; Kut. 2:23—25; Luka 7:11-16; 1 Yoh. 3:17; Yn. 11:35; Rum. 12:15; 2 Kor. 1:3,4. Fungu la Kukariri: “Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao.” (Mathayo 14:14). Lingekuwa jambo la kusikitisha kiasi gani? Msichana mwenye umri wa miaka 17 alikuwa anapambana na kile ambacho wasichana wengi wa umri huo hupambana nacho, lakini zaidi sana, msichana huyo alijinyonga. Nani angeweza kukisia huzuni kubwa iliyokuwa imewafikia wazazi wake?  ...