Machapisho

Chapisho Lililoangaziwa

Januari 26 - Mungu au Sanamu?

Mungu au Sanamu? Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu... Wazfanyao watafanana nazo, Kila mmoja anayezitumainia. Zaburi 115:4-8. Siku za Nuhu laana maradufu ilikuwa duniani ikiwa ni matokeo ya uasi wa Adamu na ya mauaji yaliyofanywa na Kaini. Hata hivyo, haya yalikuwa hayajabadilisha sana uso wa asili wa dunia. . . jamiii ya binadamu bado ilikuwa katika nguvu zake za awali. Vizazi vichache tu vilikuwa vimepita tangu Adamu alipoweza kuufikia mti ambao ulikuwa na uwezo wa kurefusha uhai; na urefu wa maisha ya mwanadamu ulikuwa bado ukipimwa kwa karne. Kama watu hawa walioishi maisha marefu wakiwa na nguvu zisizo za kawaida katika kupanga na kutenda, wangejitoa wenyewe kwa ajili ya utumishi wa Mungu, wangefanya jina la Muumba wao liwe sifa katika dunia... Lakini walishindwa kufanya hili. ... Wakiwa hawakutamani kumfanya Mungu abaki katika ujuzi wao, wakafikia hatua ya kukana kuwepo kwake. Wakatukuza viumbe ...

TUNAWEZAJE KUITAMBUA IMANI YA KWELI KATIKATI YA DINI NA MADHEHEBU MENGI SANA ULIMWENGUNI LEO?

Vitabu vyote vya dini hususani biblia na quran vinatambua na kukubaliana na ukweli kuwa mitume na manabii ndio wanaotumika kuweka mwelekeo juu ya imani halisi ya haki na ya kweli. Mafungu yafuatayo yanathibitisha nikisemacho ·         Ephesians 2:20 Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni. ·         Quran 3:84 . Sema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na tuliyo teremshiwa sisi, na aliyo teremshiwa Ibrahim, na Ismail, na Is-haak na Yaakub na wajukuu zao, na aliyo pewa Musa na Isa na Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi. Hatubagui baina yao hata mmoja, na sisi ni wenye kusilimu kwake. ·         Quran 10:19 . Wala watu hawakuwa ila Umma mmoja tu. Kisha wakakhitalifiana. Na lau kuwa si neno lililo kwisha tangulia kutokana na Mola wako Mlezi, hapana shaka hukumu ingeli kwisha katwa baina yao katika hayo wanayo khitalifiana....

januari28-Talanta Zilizotumiwa Vibaya

Talanta Zilizotumiwa Vibaya Na jina la nduguye aliitwa Yubali; huyo ndiye baba yao wapigao kinubi na filimbi. Sila naye akamzaa Tubal-kaini, mfua kila chombo cha kukatia, cha shaba na cha chuma. Mwanzo 4:21, 22. Kwenye Gharika uvumbuzi Wa sanaa na ustadi wa binadamu ulioangamia ulikuwa wa juu kuliko dunia inavyojua leo. Sanaa iliyoangamizwa ilikuwa zaidi ya sanaa inayofikiria ambayo ulimwengu unajivunia leo. ... Alipokuwa akiuangalia ulimwengu, Mungu aliona kwamba akili aliyokuwa amewapa watu ilikuwa imepotoshwa, kwamba fikra za moyo wake zilikuwa ovu wakati wote. Mungu alikuwa amewapatia watu hawa ujuzi. Alikuwa amewapatia mawazo ya thamani, ili wapate kukamilisha mpango wake. Lakini Bwana aliona kuwa wale aliowaumba ili wawe na hekima, busara na uamuzi, walikuwa wakitumia kila uwezo wa akilj zao kutukuza nafsi. Kwa kutumia maji ya Gharika, alifutilia mbali jamii hii iliyokuwa ikiishi muda mrefu kutoka katika dunia na pamoja nao ukaangamia ujuzi amba...

januari27-Majitu Katika Nchi

Majitu Katika Nchi Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile. Mwanzo 6:4. Watu wa kwanza duniani walipokea maelekezo yao kutoka kwa huyo Mungu asiye na mwisho ambaye aliiumba dunia. Wale waliopokea ujuzi wao moja kwa moja kutoka kwa hekima isiyo na mwisho hawakupungukiwa hekima... Yapo mavumbuzi mengi na maendeleo na mashine zinazofanya kazi leo ambazo watu wa kale hawakuwa nazo. Hawakuzihitaji... Watu kabla  ya gharika waliishi miaka mamia mengi na walipokuwa na umri wa miaka mia, walifikiriwa kuwa vijana tu. Wale watu walioishi maisha marefu walikuwa na akili nzuri na wenye miili mizuri... Walianza kuonekana kwenye jukwaa la shughuli katika umri wa miaka sitini hadi miaka mia moja, umri ambao kama ilivyo leo, wale ambao wameishi maisha marefu wanakuwa wamekwisha kufanya sehemu yao katika kipindi kifupi sana cha maisha na wanakuwa wameshaondoka jukwaani. Walikuwepo majitu wengi, watu warefu na wenye nguvu, waliofahamika kwa hekima, wenye ustadi...