TUNAWEZAJE KUITAMBUA IMANI YA KWELI KATIKATI YA DINI NA MADHEHEBU MENGI SANA ULIMWENGUNI LEO?

Vitabu vyote vya dini hususani biblia na quran vinatambua na kukubaliana na ukweli kuwa mitume na manabii ndio wanaotumika kuweka mwelekeo juu ya imani halisi ya haki na ya kweli. Mafungu yafuatayo yanathibitisha nikisemacho
·        Ephesians 2:20Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.

·        Quran 3:84. Sema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na tuliyo teremshiwa sisi, na aliyo teremshiwa Ibrahim, na Ismail, na Is-haak na Yaakub na wajukuu zao, na aliyo pewa Musa na Isa na Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi. Hatubagui baina yao hata mmoja, na sisi ni wenye kusilimu kwake.

·        Quran 10:19. Wala watu hawakuwa ila Umma mmoja tu. Kisha wakakhitalifiana. Na lau kuwa si neno lililo kwisha tangulia kutokana na Mola wako Mlezi, hapana shaka hukumu ingeli kwisha katwa baina yao katika hayo wanayo khitalifiana.

·        Hii ina maana kwamba“Watu wote walikuwa na dini moja aliyokuja nayo nabii Adam kisha wakahitilafiana” Na ndivyo isomekavyo pia katika machapisho mengine ya Qur an.

·        Yeremiah 6:16 Bwana asema hivi, Simamenikatikanjiakuu, mkaone, mkaulize habari za mapito ya zamani, I wapi njia iliyo njema? Mkaende katikanjia hiyo, nanyi mtajipatia raha katika nafsi zenu. Lakini walisema, Hatutaki kwenda katikanjia hiyo.
Maandiko haya yamefunua wazi kile nilichokisema kwamba manabii na mitume ndio njia ya pekee na rahisi kwa kutuonyesha ndini ya kweli na sahihi.Tunamshukuru sana Mungu kwa kutusaidia katika hili kwa sababu ingekuwa ni kazi ngumu kuliko kupanda mlima mrefu sana kuitambua dini ya kweli na sahihi. Hili linatupa uhakika wa kuipata dini ya kweli hata katika wimbi la dini na madhehebu mengi sana ulimwenguni leo.
Andiko lifuatalo linathibitisha zaidi dai hili;
Quran 42:13. Amekuamrisheni Dini ile ile aliyo muusia Nuhu na tuliyo kufunulia wewe, na tuliyo wausia Ibrahim na Musa na Isa, kwamba shikeni Dini wala msifarikiane kwayo. Ni magumu kwa washirikina hayo unayo waitia. Mwenyezi Mungu humteua kwake amtakaye, na humwongoa kwake aelekeaye. Linganisha na yeremia 6:17.
Hivyo mapito sahihi ni katika njia ile ile waliyopita akina Ibrahimu,Musa,Isa na manabii wengine wote maana maandiko yako bayana kwamba dini iliyoamrishwa ni moja peke yake. Nitaonyesha baadae kidogo hawa manabii walishika njia ipi katika kumwelekea Mungu ili tupate nuru kubwa na kuchuma maarifa ya kuitambua imani sahihi. Tuihoji Qur an kama inatambua kuwepo kwa kundi la wakristo.
LIPO KUNDI LA WAKRISTO NA JE NI SAHIHI KUWEPO?
Quran 3:110. Nyinyi mmekuwa bora ya umma walio tolewa watu, kwa kuwa mnaamrisha mema na mnakataza maovu, na mnamuamini Mwenyezi Mungu. Na lau kuwa Watu wa Kitabu nao wameamini ingeli kuwa bora kwao. Wapo miongoni mwao waumini, lakini wengi wao wapotovu.
Quran 3:55. Pale Mwenyezi Mungu alipo sema: Ewe Isa! Mimi nitakufisha, na nitakunyanyua kwangu, na nitakutakasa na wale walio kufuru, na nitawaweka wale walio kufuata juu ya wale walio kufuru, mpaka Siku ya Kiyama. Kisha marejeo yenu yatakuwa kwangu, nikuhukumuni katika yale mliyo kuwa mkikhitalifiana.
Qur an imeweka bayana uwepo wa kundi la wakristo ingawa inakiri kuwa wengi wao walipotoka na hivyo kuiacha njia iliyo sahihi. Kilichonishangaza zaidi ndugu zangu nikuona namna Qur an inavyoliweka kundi la wafuasi wa Yesu juu ya wote mpaka siku ya mwisho.
Kama mtu atakuwa ameweka itikadi yake pembeni na kutafakari kwa kina mambo haya yazungumzwayo na vitabu hivi atakuwa ameanza kupata picha ya kile kisemwacho ambao ni ukweli mtupu.
Biblia inasema katika Matendo 11:26 kwambahata alipokwisha kumwona akamletaAntiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa nakuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwaWakristokwanza hapo Antiokia”.
Hivyo wafuasi wa Bwana Yesu wanaitwa wakristo na ndio ambao kiukweli watawekwa juu ya wengine wote mpaka siku ya kiama kama pia Qur an inavyiripoti. Kama hiyo haitoshi; Katika Quran 41:61 msaafu unasema “Na kwa hakika yeye ni alama ya Saa ya Kiyama. Basi usiitilie shaka, na nifuateni. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka”. Maneno kuwa yeye ni njia yanaungwa mkono pia na Injili yake katika yohana 14:6 isemapo “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”.Hakuna alama nyingine ya saa ya kiama.Chukua tahadhari mpendwa na ufanye maamuzi ya kweli na sahihi hata kama ni kwa gharama kubwa.
Katika kile kinachosemwa na Qur an kuhusu kuhitilafiana kwa wakristo, hata nabii Daniel alikiona na akasema mamlaka ya pembe ndogo itaazimu kubadili majira na sheria.Kitabu cha Danieli 7 kinatoa unabii ya falme nne zilizowahi kutawala dunia;kwa macho ya kiroho Danieli akionyeshwa kabla hazijatokea.Aliziona kwa mfano wa wanyama wanne ambao ni simba,dubu,chui na mnyama wa kutisha.
Simba iliwakilisha Babeli, Dubu-Umedi na Uajemi,Chui-Ugiriki ama Uyunani na mnyama wa kutisha ni Rumi. Baada ya Rumi kusambaratika katika mwaka wa 476 BK ndipo tukapata mataifa kumi, saba yakiwepo mpaka  leo na ndiyo yanayotengeneza sehemu kubwa ya bara la Ulaya(uingereza,ufaransa,ubeligiji,ujerumani,ureno,Hispania na Italia).Tatu ziling’olewa kabisa(vandals,ostrogoth na heruli).
Kutoka kwenye mataifa haya 10 ilitokea mamlaka nyingine ambayo ilikuwa tofauti na zingine zote kwa kuwa hii ilikuwa na kinywa kilichonena maneno makuu ya makufuru na hivyo kuonyesha kuwa ilikuwa na nguvu ya kidini maana kukufuru kunahusiana na dini na siyo siasa.Kanisa katoliki na uongozi wake lilifanya nikisemacho kwamba lilibadili majira na sheria za Mungu na hivyo ndio pembe ndogo kama isemwavyo katika Dan.7:25. ATAAZIMU KUBADILI MAJIRA NA SHERIA.
Amri za Mungu kama zisemwavyo na biblia ni tofauti na zilivyoandikwa katika katekisimu zao.Amri ya pili inayozuia kujifanyia sanamu za kuchonga imeondolewa, kisha wakaibadili amri ya nne ya sabato na kusomeka shika kitakatifu siku ya Bwana.
Swali: Hicho kitakatifu ni kinini? Siku ya Bwana ni ipi?. Katika biblia amri hiyo inasema“Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yotelakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana, kwa siku sita Bwana alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo Bwana akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa”.Kama hiyo haitoshi wakaigawa amri ya kumi inayozuia tamaa mara mbili ili kupata idadi kamili ya amri 10 kwa kuwa wameiondoa amri ya pili!
Nithitibitisha hili kwa kutumia vitabu vyao wenyewe.
·        No such law in the Bible "Nowhere" in the bible do we find that Jesus or the apostles ordered that the Sabbath be changed from Saturday to Sunday. We have the commandment of God given to Moses to keep holy the Sabbath day, that is, the Seventh day of the week, Saturday. Today, all Christians keep Sunday because it has been revealed to us by the [Roman] church outside the Bible." Catholic Virginian, Oct. 3, 1947 (Hakuna sheria hiyo popote pale kwenye biblia tunayoweza kupata kwamba Yesu au mitume waliamuru kubadilishwa kwa sabato kutoka jumamosi kwenda jumapili.Tuna amri ya Mungu aliyompatia Musa inayotutaka kuitakasa siku ya sabato,yaani siku ya saba ya wiki,jumamosi.Leo wakristo wote huishika jumapili kwa sababu imefunuliwa kwetu na kanisa la katoriki,nje ya biblia)

·        "You may read the Bible from Genesis to Revelation, and you will not find a single line authorizing the sanctification of Sunday. The Scriptures enforce the religious observance of Saturday, a day which we never sanctified." James Cardinal Gibbons, The Faith of Our Fathers (1917 ed.), pp.72,73.(Unaweza kusoma biblia kutoka mwanzo mpaka ufunuo na hutapata msitari hata mmoja unaoidhinisha utakaswaji wa jumapili.Maandiko yanaagiza kuitunza jumamosi,siku ambayo hatukuitakasa)

·        "If protestants would follow the Bible, they should worship God on the Sabbath Day, that is Saturday. In keeping Sunday they are following a lawof the Catholic Church." Albert Smith, chancellor of the Archdiocese of Baltimore, replying for the cardinal in a letter of Feb. 10, 1920.(Kama walokole wangefuata biblia,wanatakiwa kumwabudu Mungu siku ya sabato,yaani jumamosi. Kwa kuitunza jumapili,wanafuata sheria ya kanisa katoliki)
·        Peter Geiermann, C.S.S.R., The Converts Catechism of Catholic Doctrine (1957), p. 50.
"Question: Which is the Sabbath day?
"Answer: Saturday is the Sabbath day.
"Question: Why do we observe Sunday instead of Saturday?
"Answer. We observe Sunday instead of Saturday because the Catholic Church transferred the solemnity from Saturday to Sunday."
·        Swali: Siku ya sabato ni ipi?
·        Jibu: Jumamosi ni siku ya sabato
·        Swali:Kwa nini tunaiadhimisha jumapili badala ya jumamosi?
·        Jibu: Tunaadhimisha jumapili badala ya jumamosi kwa sababu kanisa katoliki lilihamisha utukufu kutoka jumamosi kwenda jumapili.MWISHO WA KUNUKUU.
Hapa sasa tunapata uhakika mwingine wa nani chanzo cha kuhitilafiana kwa wakristo. Wakati wa Yesu na mitume watu wote walikuwa wakiitunza sabato ya Bwana,siku ya saba yaani jumamosi.Taratibu taratibu ukengeufu ukaanza kuingia kanisani na watu wakaanza kuiacha njia iliyonyoka ya mapito ya mitume na manabii.
Ikawa watu wakaanza kuabudu jumamosi na jumapili na ilipofika mwaka wa 321BK mfalme Constantine wa Rumi akatoa amri ya kuabudu siku ya jumapili katika dola yake yote.Hapo ndipo kanisa katoliki linapopata nguvu.Hata hivyo baadae waumini wa kanisa hili wakaanza kuhitilafiana tena kwa kile ambacho kilionekana kuwa kiini macho kwa waumini.Kanisa  lilifundisha na kuwataka watu kupokea msamaha wa dhambi kutoka kwa papa huku hawaoni madai hayo kwenye biblia,ndipo watu Kama Martin Luther walipoamua kujitenga na kanisa na wafuasi wake wakajiita walutheri, Baadae tena waanglikan na madhehebu mengine mengi yakameguka.
Ndivyo kulivyo kumeguka na kuhitilafiana kwa makanisa kulivyotokea kama inavyoripotiwa na Qur an pia kwamba walihitilafiana. Njia na mapito sahihi ni ile ya zamani ambayo tumeiona kuwa ilikuwa ya mitume na manabii pia na hakuna mabadiliko yatakayokuja kutokea. Sabato ilikuwepo tangu mwanzo wa kuumbwa kwa sayari Dunia. Mwanzo 2:1-3 “1 Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote. 2 Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya. 3 Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya”.
Hata kalenda ya kiarabu itumikayo kuhesabu siku kama itambuliwavyo na waislamu inasaidia kuthibitisha kile nikisemacho na kuonyesha kuwa kweli jumamosi ndiyo siku ya saba.

Jumapili: yaum al-ahad (siku ya kwanza) يوم الأحد
Jumatatu: yaum al-ithnayna (siku ya pili) يوم الإثنين
Jumanne: yaum ath-thalatha (siku ya tatu) يوم الثلاثاء
Jumatano: yaum al-arba`a (siku ya nne) يوم الأَربعاء
Alhamisi: yaum al-khamis (siku ya tano) يوم خميس
Ijumaa: yaum al-jum`a (siku ya mkutano) يوم الجمعة
Jumamosi: yaum as-sabt (siku ya sabato)يوم السبت


Quran 3:71 inasema, Enyi Watu wa Kitabu! Mbona kweli mnaivisha uwongo, na kweli mnaificha na hali mnajua?
Hapa inadhihirisha madai kuwa ni kweli sabato iligeuzwa na hawa wakristo waliokuwa wanajua ukweli ila wakaamua kuuvisha uongo.Ili kupona kwao kuje wanatakiwa kuyarejea mapito ya zamani ya mitume na manabii ya kuabudu na kuitunza sabato ya Bwana kama ilivyoamuriwa na vitabu vyote vya dini hizi.Hili pia linathibitishwa na fungu lifuatalo;
Quran 5: 68. Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Hamna lenu jambo mpaka muishike Taurati na Injili na yote mlio teremshiwa kutokana na Mola wenu Mlezi. Na hakika ulio teremshiwa wewe kutokana na Mola wako Mlezi yatawazidishia wengi katika wao uasi na ukafiri. Basi usiwasikitikie watu makafiri.
Baada ya mpasuko wa hawa wakristo,kuna wapo waliobaki imara?
Quran 9:29. Piganeni na wasio muamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho, wala hawaharimishi alivyo harimisha Mwenyezi Mungu na Mtume, wala hawashiki Dini ya Haki, miongoni mwa walio pewa Kitabu, mpaka watoe kodi kwa khiari yao, hali wamet'ii.
Hapa jambo linawekwa sawa kwamba kuna miongoni mwa waliopewa kitabu(wakristo) ambao hawaharimishi alivyoharamisha mwenyezi Mungu.Hii inaonyesha si wote,kumbe kuna waliobakia kuwa waaminifu.Amri hii ilitolewa na Abubaker alipokuwa ameyakusanya makabila ya kiarabu kwa ajili ya vita dhidi ya rumi ya mashariki waliambiwa kudhuru wote waabudu sanamu na kuwaacha wote wacha Mungu wa kweli.Na hili ndilo kundi ambalo nalizungumzia kuwa wametunza maagizo ya Bwana tangu zamani. Ukweli ni kwamba kwenye kila kizazi, kumekuwepo waaminifu wa kweli ambao wamezitunza amri zote 10 za Mungu kwa gharama yoyote ile. Wengi walimwaga damu kwa kuwa watiifu kwa Mungu.
Rumi ya kidini chini ya uongozi wa upapa kuanzia mwaka 538 BK mpaka 1798 BK ilitawala dunia na kuua mamilioni ya watu waliopingana na mafundisho yake.Historia inaonyesha kwamba zaidi ya watu milioni 50 waliuawa na mkono huu.Hakuna mauaji yaliyowahi kufanyika kama haya tangu kuwepo kwa dunia.Kipindi hiki kinaitwa DARK AGE na biblia ilipigwa marufuku kusomwa wala kuuzwa. Nitaeleza habari hizi zaidi katika waraka wangu mwingine.
DINI YA MITUME NA MANABII NI IPI SASA?
Tangu mwanzo,manabii na mitume wote wamekuwa wakiishika na kuitunza sabato ya Bwana.Sabato ni amri ya Mungu aliyoitoa mwenyewe,akaiandika kwa chanda chake mwenyewe na nabii Ibrahimu akashika amri za Mungu ikiwepo nah ii pia.Mwanzo 26:5 inasema “Kwa sababu Ibrahimu alisikia sauti yangu, akayahifadhi maagizo yangu, na amri zangu, na hukumu zangu, na sheria zangu”. Napa Ibrahimu aliitii sabato kwa sababu Mungu asingesema kuwa alihifadhi sheria zake kama angevunja hata iliyo moja. Yakobo anatusaidia katika hili kwamba ukivunja amri 1, umevunja zote(yakobo 2:10)-Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote.Hivyo ni kusema Ibrahimu alizishika sheria na amri zote za Mungu ikiwepo ya sabato.
MUSA-huyu ndiye mpokeaji wa amri zote.Baada ya Mungu kuziandika kwa chanda chake mwenyewe alimkabidhi Musa kuwafikishia wana wa Israel na hakuna shaka kuwa nabii huyu alikuwa mtiifu wa amri za Mungu ikiwepo na SABATO.( Kumbukumbu la torati 4:13 Akawahubiri agano lake, alilowaamuru kulitenda, yaani, zile amri kumi; akaziandika juu ya mbaombili za mawe)
Kumbukumbu la torati  5:22 Haya ndiyo maneno ambayo Bwana aliwaambia mkutano wenu wote mlimani kwa sauti kuu toka kati ya moto, na wingu, na giza kuu; wala hakuongeza neno. Akayaandika juu ya mbaombili za mawe, akanipa.
Matendo 15:21 Kwa maana tangu zamani za kale Musa anao watu wahubirio mambo yake; katika kila mji husomwa kila sabato katika masinagogi. Ni wazi kabisa kwamba kumbe sabato imekuwepo tangu zamani na manabii waliitii.
YESU(ISA )-Huyu nae ilikuwa desturi yake kuishika sabato kama inavyowekwa bayana katika luka 4:16 ikisema Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; na siku ya sabato akaingia katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake, akasimama ili asome.Desturi ni kawaida au tamaduni.ilikuwa hivyo kwake siku zote.
Matendo 13:27 Kwa maana wakaao Yerusalemu, na wakuu wao, kwa kuwa hawakumjua yeye, wala maneno ya manabii yanayosomwa kila sabato, wameyatimiza kwa kumhukumu. Kumbe manabii waliizingatia sabato kama lisemavyo fungu hili kwa uwazi kabisa.
MITUME WA YESU VIPI?
·        Matendo 16:13 Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani ya kuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale
·        Matendo 17:2 Na Paulo, kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko sabato tatu
·        Matendo 18:4 Akatoa hoja zake katika sinagogi kila sabato, akajaribu kuwavuta Wayahudi na Wayunani
·        Matendo 13:14 Lakini wao wakatoka Perge, wakapita kati ya nchi, wakafika Antiokia, mji wa Pisidia, wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi.
Mafungu haya yote yanaonyesha namna ambavyo mitume walikuwa wakiitunza sabato ya Bwana.Wewe vipi mpendwa?
Kuthibitisha zaidi kuwa sabato iliheshimiwa tangu zamani, hata Quran ilipokuja ililipoti kitu hicho.
Quran 7: 163. Na waulize khabari za mji ulio kuwa kando ya bahari, wakiivunja Sabato (Jumaamosi ya mapumziko). Samaki walikuwa wakiwajia juu juu siku ya mapumziko yao, na siku zisio kuwa za kupumzika hawakuwa wakiwajia. Kwa namna hiyo tuliwajaribu kwa sababu walikuwa wakifanya upotovu.
Kutoka 20:8-11(Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.Maana, kwa siku sita Bwana alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo Bwana akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa).
Quran 4:47 Enyi mlio pewa Kitabu! Aminini tuliyo yateremsha yenye kusadikisha yale mliyo nayo, kabla hatujazigeuza nyuso tukazipeleka kisogoni, au tukawalaani kama tulivyo walaani watu wa Sabato (Jumaamosi). Na amri ya Mwenyezi Mungu ni lazima ifanyike.
Waliolaaniwa ni wale walioivunja sabato na ndio maana katika fungu lifuatalo likasisitiza hicho;
Quran 2:65. Na hakika mlikwisha yajua ya wale miongoni mwenu walio ivunja Sabato,(siku ya mapumziko, Jumaa Mosi) na tukawaambia:Kuweni manyani wadhalilifu.
Kiukweli sioni lugha ngumu na kali kama hii iliyotumika kuwaita wavunja sabato ya Bwana na pia sioni ugumu wa moyo wa yeyote Yule kuendelea kuipinga sabato ya Bwana.Fanya maamuzi ya kweli ndugu yangu tuokolewe.Suala la wokovu ni la mtu mwenyewe siyo familia wala rafiki maana kila mtu atasimama mwenyewe siku ya hukum
Quran 4:154. Na tukanyanyua mlima juu yao kwa kufanya agano nao. Na tukawaambia: Ingilieni mlangoni kwa unyenyekevu. Na tukawaambia: Msiivunje Siku ya Sabato (Jumaa mosi). Na tukachukua kwao ahadi iliyo madhubuti.
Quran 16:124. Hakika siku ya Sabato (Jumaamosi) waliwekewa wale walio khitalifiana kwa ajili yake. Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka atahukumu baina yao Siku ya Kiyama katika yale waliyo kuwa wakikhitalifiana
IJUMAA IMETOKA WAPI?
Quran 17: 77. Huo ndio mwendo kwa Mitume tulio watuma kabla yako. Wala hupati mabadiliko katika mwendo wetu.linganisha pia na quran 3:84 tuliyokwisha kuiona.
Hapa tunaona kuwa mabadiliko ya mitume si kigezo cha kubadili mafunuo na amri za Mungu.Zingatia sentensi iliyopigiwa mstari hapo juu.
Historia inaonyesha kwamba mtume Mohammad alikuwa akifanya sala kwa kuangalia upande wa Yerusalemu(Baytil Muqaddas) kwa muda wa mwaka mmoja na nusu.Inaonyesha kuwa alikuwa akiijua vizuri dini ya kikristo kwa kuwa hata akina Danieli walifanya hivyo.Soma fungu hili;
Quran 2: 144. Kwa yakini tukiona unavyo geuza geuza uso wako mbinguni. Basi tutakuelekeza kwenye Kibla ukipendacho. Basi elekeza uso wako upande wa Msikiti Mtakatifu; na popote mnapokuwa zielekezeni nyuso zenu upande huo; na hakika wale walio pewa Kitabu wanajua kwamba hiyo ni haki itokayo kwa Mola wao Mlezi. Na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na yale wanayo yatenda.Danieli 6:10 inasema Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.
Katika pango la jabal ilaa mwaka wa 610 BK ndipo mabadiliko mengi yakaja kwa mtume ikiwepo na sala ya ijumaa ambayo ilianza rasmi mwaka 622BK
Quran 2: 145. Na hao walio pewa Kitabu, hata ukiwaletea hoja za kila namna, hawatafuata Kibla chako; wala wewe hutafuata kibla chao, wala baadhi yaohawatafuata kibla cha wengineo; na kama ukiyafuata matamanio yao baada ya kukufikia ujuzi, hakika hapo utakuwa miongoni mwa wenye kudhulumu.
Mtume kwa mara ya kwanza aliswali swala ya ijumaa katika maskani ya Bani Salim bin Awf katika wangwa wa Ronunaa.Alikuwa katika safari yake kwenda madina akitokea makka.
Ibada ya ijumaa haibebi sifa ya jumamosi na hata hivyo imetajwa mara moja tu katika Qur an nzima napo ikiwa haikatazi kabisa kufanya kazi siku hiyo, lakini jumamosi ni siku ya kuadhimisha matendo ya ibada tu.Tuisome iyo aya;Quran 62:9-10 inasema  Enyi mlio amini! Ikiadhiniwa Sala siku ya Ijumaa, nendeni upesi kwenye dhikri ya Mwenyezi Mungu, na wacheni biashara. Hayo ni bora kwenu, lau kama mnajua.
10. Na itakapo kwisha Sala, tawanyikeni katika nchi mtafute fadhila za Mwenyezi Mungu, na mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi ili mpate kufanikiwa.
Unaona? Haijakataza kufanya kazi ilihali Mungu alitupatia kielelezo cha namna ya kuenenda kupitia kazi yake ya uumbaji; Kwamba aliumba kwa siku sita kasha akapumzika kama ilivyosemwa katika biblia lakini pia katika Qur an 7:54  Hakika Mola Mlezi wenu ni Mwenyezi Mungu aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kisha akatawala juu ya Kiti cha Enzi. Huufunika usiku kwa mchana, ufuatao upesi upesi. Na jua, na mwezi, na nyota zinazo tumika kwa amri yake. Fahamuni! Kuumba na amri ni zake. Ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote. Soma pia KUTOKA 20:11 uone kufanana kwake.
Wapo watu wasemao kuwa amri ya sabato iliwahusu wayahudi peke yao! Nami nauliza swali?
·        Je, kuiba,kusema uongo, kuzini, kutokuwaheshimu wazazi kunaruhusiwa leo kwa kuwa hizi nazo zilikuwa za wayahudi?
·        Ina maana gani yesu kusema katika marko 2:27 kwamba sabato ilifanyika kwa ajili ya wanadamu?
Ukweli ni kwamba watu wanajifariji tu kwa madai haya.Ukweli utaendelea kudumu mpaka mwisho wa wakati.Amri ya sabato ni mhuri wa Mungu mwenyewe.Ni ishara ya utakaso, ukombozi na mamlaka yake ya uumbaji.
SABATO ITADUMU MILELE.HATA MBINGUNI ITATUNZWA KWA KICHO SANA NA VIUMBE VYOTE (ISAYA 66:22-24).
IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.
Isikie sauti ya Mungu usiwe mtu mwenye masikio asiyesikia. Mungu awatangulie mtafakaripo maneno haya ya uzima.AMEN!
Nimetumia Biblia, Qur an na vitabu vingine vya dini pamoja na vya historia kuuthibitisha ukweli huu ambao watu wengi hawapendi kuusema. Msaafu wa Qur an umeweka bayana sana suala hili kama ilivyo kwa biblia pia.

KUMBUKA DUNIA INA MWISHO WAKE.YESU ANAKUJA TENA.YEYE NI SAA YA ALAMA YA KIAMA.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Somo 8:Yesu Alionesha Huruma Agosti 13-19,2016

Kesha la Asubuhi Agosti 6- 12,2016