Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2016

Kuwahubiri wauaji Sehemu ya II-Somo toka Rwanda

Picha
Na Fodidas Ndamyumugabe Kumbuka: Fodidasi amekamatwa na wauaji, waliomwamuru ajichimbie kaburi lake mwenyewe. Kadri aliyochimba kaburi, mmoja wa wauaji hao alivutiwa na Biblia ya Fodidasi na kuanza kumwuliza maswali. Mara baada ya kaburi kuchimbwa ,kundi hilo la wauaji liliamua kutumia kaburi hilo kumzika mtu mwingine. Kabla ya kumwamuru Fodidasi kuchimba kaburi la pili, walimpatia wasaa apate kuwahubiri. Kwanza ninawashukuru sana. “Ahsanteni kwa kufanya dua kwa ajili ya mtu mliyemwua. Hata hivyo mwapaswa mjue Biblia isemacho kuhusu kifo—wasaa pekee ambapo waweza kuokolewa ni wakati ukingali hai—siyo baada ya kifo. “ Kwa sababu walio hai wanajua kuwa watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote ” Mhubiri 9:5. “Sitawasihi kuwa mniachie hai,” aliendelea kujieleza, “kwa sababu najua hata mkiniua muda utafika ambapo nitafufuliwa.” “Miongofli mwa watu mnaowaua ni wa makabila mengine—siyo Wahutu au Watusi. Ni watoto wa Mungu. Mnafikiri mnapambana vita ya kikabila, ila mmekosea. H...

Kuwahubiri wauaji -Sehemu ya Kwanza

Picha
somo toka Rwanda Na  Fodidas Ndamyumugabe Kisa cha  msamaha na kusameheana kwa wahanga wa mauaji wa kimbari nchini Rwanda yaliyotokea mwaka 1994. Ni matukio halisi, yenye kusikitisha na kuvuta hisia kwa kiasi kikubwa.          Fodidasi-ambaye jina lake humaanisha “Ninamwabudu BWANA” alizaliwa katika kaya ya Kiadventista  iliyokuwa ikiishi milimani huko Rwanda. Tangia ujana wake  alionesha kuwa ana kipaji cha uongozi, akajitoa kumtumikia Bwana. Alikuwa na bidii katika chama cha Watafuta njia na hatimaye katika chama cha Vijana. Alikuwa mlezi mwema wa kiroho wa vijana wenzake ,na kuongoza ibada asubuhi shuleni mwao kila siku.          Kadiri miaka ilivyosogea Biblia yake ilikuwa imepigiwa mistari kila mahali kuonesha aliisoma kwa bidii. Fodidasi hakujua ni kwa jinsi gani Biblia hiyo itaokoa maisha yake mnamo vita vya kimbari mwaka 1994 pale alipohitajika kuwahubiri Wauaji. K...

Ufunuo wa Yohana

Picha
                                                  Kulikuwa na Vita Mbinguni;Mikaeli na Malaika zake wakapigana na yule joka,yule joka  naye akapigana nao pamoja na malaika zake;nao hawakushinda,wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa,nyoka wa zamani,aitwaye ibilisi na shetani,audanganyaye ulimwengu wote;akatupwa hata nchi,na malaika zake wakatupwa pamoja naye. Nikasikia sauti kuu mbinguni,ikisema,Sasa kumekuwa wokovu,na nguvu,na ufalme wa Mungu wetu,na mamlaka ya Kristo wake;kwa maana ametupwa  chini mshitaki wa ndugu zetu,yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.Nao wakamshinda kwa damu ya mwana kondoo,na kwa neno la ushuhuda wao,ambao hawakuyapenda maisha yao hata kufa.   Kwa hiyo shangilieni,enyi mbingu,nanyi mkaao humo.Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu ny...

Lesson Agosti 27-Sept 2,2016

Picha
Somo la 10                                                Agosti 27 — Septemba 2   Yesu Aliwafanya Wamwamini   Usomaji wa Biblia: Ezra 10   Sabato Mchana   Soma kwa Ajili ya Somo la Juma Hili: Mwa. 15:6; Hes. 11:4; 1 Kor. 3:1-9;   Dan. 6:1-3; Neh. 2:1-9; Kum. 4:1-9; Mdo. 2:42-47.   Fungu la Kukariri: “Lakini habari zake zikazidi kuenea, wakakutanika makutano mengi wamsikilize na kuponywa magonjwa yao.” (Luka5:15). K wa miaka kadhaa, Kanisa moja la Waadventista wa Sabato limekuwa likitoa kifungua kinywa siku tano kwa juma kwa shule ya awali ya mahali pale. Ijapokuwa serikali ya taifa lile ilikuwa ya kiraia kabisa (haikuwa ya kidini), ililazimika kupitisha sheria ili kutoa pesa ya kutosha k...

Kesha la Asubuhi agosti 27-sept 2,2016

Agosti 27 Tunabeba Msalaba na Kujikana Nafsi Nimesulubiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo ya hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu. Wagalatia 2:20.         Kristo alisulubiwa kwa ajili ya mwanadamu aliyeanguka dhambini. Lakini kwa wengi wanaojiita kuwa ni Wakristo, tukio hili halina maana yoyote. Kwa matendo, wanaukana msalaba wa Kristo ... Wanakubali kuwa Kristo alikufa msalabani, lakini kwa sababu kuna uzoefu wa kusulubiwa ambao inawapasa waupitie, hawapokei mafundisho yatakayowafanya wajikane nafsi na kujitoa. Hawa ni Wakristo kwa jina tu. Kiini cha imani yao sio Mwokozi aliyesulubiwa, anayewaletea wote wanaompokea fadhila ya kuwa wana na binti za Mungu.         Acha anasa za dhambi na badala yake uichukue mbingu na uzima wa milele. Siku chache...