Ufunuo wa Yohana

                                                 

Kulikuwa na Vita Mbinguni;Mikaeli na Malaika zake wakapigana na yule joka,yule joka  naye akapigana nao pamoja na malaika zake;nao hawakushinda,wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.
Yule joka akatupwa,nyoka wa zamani,aitwaye ibilisi na shetani,audanganyaye ulimwengu wote;akatupwa hata nchi,na malaika zake wakatupwa pamoja naye.
Nikasikia sauti kuu mbinguni,ikisema,Sasa kumekuwa wokovu,na nguvu,na ufalme wa Mungu wetu,na mamlaka ya Kristo wake;kwa maana ametupwa  chini mshitaki wa ndugu zetu,yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.Nao wakamshinda kwa damu ya mwana kondoo,na kwa neno la ushuhuda wao,ambao hawakuyapenda maisha yao hata kufa.
  Kwa hiyo shangilieni,enyi mbingu,nanyi mkaao humo.Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.
Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi,alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanaume.
Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa ,ili aruke,aende zake nyikani hata mahali pake,hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati,mbali na nyoka huyo.
Nyoka akatoa katika kinywa chake ,nyuma ya huyo mwanamke,maji kama mto,amfanye kuchukuliwa na mto ule.
Nchi ikamsaidia mwanamke;nchi ikafunua kinywa chake,ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.Joka akamkasilikia yule mwanamke,akaenda zake afanya vita juu ya wazao wake waliosalia,wazishikao amri za Mungu,na kuwa na ushuhuda wa Yesu;naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.
Nukuu yote hii imetoka Ufunuo 12,fungu la 7 hadi 17
Inaeleza kulikuwa na  Vita Mbinguni kati ya Miakaeli(Yesu) na malaika zake wakapigana na shetani na malaika zake(mapepo).Imeeleza Shetani hakushinda sabubu yeye ndiyo alianzisha hiyo vita,Mbinguni kulikuwa amani yeye ndiyo alianzisha vita;
Fundisho fupi kidogo” Inaweza kukawepo amani katika familia,taasisi,kikundi fulani lakini akatokea mtu akaanzisha kitu cha kuleta mvurugano,hiyo tabia aliasisi shetani”
Shetani alishindwa hiyo vita akatupwa chini.Shetani alipapenda sana mbinguni ndiyo maana alikasilika sana kutupwa chini.Wanadamu tunaonywa Shetani alishuka mwenye ghadhabu nyingi anafanya kazi kwa bidii ya kuteka wanadamu akijua muda wake ni mchache tu.

Shetani alipoona ya kuwa ametupwa alimkasilikia mwanamke aliye mzaa mtoto Mwananume.
Maana ya mwanamke Ni kanisa.
Mtoto mwanaume –Ni Yesu Kristo.
Kanisa lenye kushika amri za Mungu zote na kuwa na ushuhuda wa Yesu Kristo ndiyo alianza kupambana nalo Ibilisi ili watu wengi wasiende mbinguni alikofukuzwa yeye.
Kazi yake ni kuharibu mipango ya Bwana,Mungu wetu.

Nyoka akatoa katika kinywa chake ,nyuma ya huyo mwanamke,maji kama mto,amfanye kuchukuliwa na mto ule.

Maana yake ni kwamba shetani akatoa mafundisho ya uongo.Hapa ndipo chimbuko la dini nyingi nyingi duniani ili ukweli usijulikane ni upi.Lengo lake ni kuwa mafundisho ya uongo yaumeze ukweli.Aliona kupambana na Imani ya Kikristo ni kujifanaisha nayo.Hapa ndipo unapata wahubiri wanaenda kupata nguvu za kufanya ishara kwa shetani,kutoa pepo na kadharika.Ukiwakuta kwenye jukwaa wanamhubiri Kristo,Kumbe ni mawakala wa shetani.
Mungu alilisaidia kanisa lake ili ukweli usipotee,ndiyo maana mpaka leo ukweli upo bayana na udanganyifu wa shetani upo bayana.

“akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia,wazishikao amri za Mungu,na kuwa na ushuhuda wa Yesu;naye akasimama juu ya mchanga wa bahari”
Shetani anafanya vita na wazao wa mwanamke waliosalio(maana yake ni wachache waujuao ukweli)
Wazishikao amri za Mungu na kuwa na ushuhuda wa Kristo.
Makanisa mengi yanaushuhuda wa Yesu tu pasipo kuzishika amri za Mungu zote alizopewa Nabii Musa.
Masalia Wa Mungu ni wale Wazishikao amri za Mungu  na kuwa na Ushuhuda Wa Yesu Kristo.
Amri za Mungu zinapatikana katika Kitabu cha Kutoka 20
1.   Usiwe na Miungu mingine ila mimi
2.   Usijifanyie sanamu ya kuchonga wala mfano wa kitu chochote kilicho juu Mbinguni,wala kilicho duniani,walakilcho majini chini ya dunia.Usivisujudie wala kuvitumikia
3.   Usilitaje bure jina la Bwana ,Mungu wako.
4.   Ikumbuke siku ya sabato uitakase.Siku sita fanya kazi utende mambo yako yote.lakini siku ya saba ni sabato ya Bwana,Mungu Wako.(Lengo la kushika sabato ni kufanya kumbukumbu kwamba Mungu ndiye aliyeiumba dunia.Laiti wanadamu wangeishika hii amri ingewakumbusha wao wameumbwa na Bwana ,Mungu wao na kila kitu wanachokiona kimetokana na Mungu na maisha yao binafsi yametoka kwa Mungu )
5.   Waheshimu baba yako na mama yako;siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi.
6.   Usiue
7.   Usizini
8.   Usiibe
9.   Usimshuhudie jirani yako uongo
10.   Usiitamani nyumba ya jirani yako,usimtamani mke wa jirani yako;wala mtumwa wake,wala mjakazi wake,wala ng’ombe wake,wala punda wake,wala usitamani chochote alicho nacho jirani yako.

Walimwengu wengi hawaishiki amri ya nne.
naye akasimama juu ya mchanga wa bahari”
Mchanga wa bahari ni watu wengi.
Shetani akasimamama juu ya mchanga wa bahari-maana yake ni watu wengi wanayafuata mafundisho Yake.

Hii inafana na pale aliposema Yesu Kristo “Njia ya kwenda upotevuni ni pana na ni wengi waipitao  na njia yakwenda Uzimani ni nyembamba na ni wachache waionayo”

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Somo 8:Yesu Alionesha Huruma Agosti 13-19,2016

Kesha la Asubuhi Agosti 6- 12,2016

TUNAWEZAJE KUITAMBUA IMANI YA KWELI KATIKATI YA DINI NA MADHEHEBU MENGI SANA ULIMWENGUNI LEO?